Taasisi ya afya ya Yohana Wavenza

Taasisi ya afya ya Yohana Wavenza ni chuo cha uuguzi ambacho kilianzishwa mwaka 2011. Kinapatikana kwenye eneo la Hospitali ya Mbozi misheni. Mafunzo ya kwanza yalianza mwezi Septemba 2011 na wanafunzi wapatao 85. Leo, zaidi ya wanafunzi 180 wamejiunga na taasisi yetu na walimu 7 hutoa mafunzo yenye ubora. Tunatoa kozi ya diploma ya uuguzi na ukunga kwa miaka mitatu.

Vifaa

Tunatoa vifaa mbalimbali vyenye lengo la kuhakikisha mazingira bora ya kujifunzia wanafunzi wetu. Kama vile, chumba cha kompyuta, maktaba na mabweni kwa wanafunzi wa kiume na wa kike.

Mtazamo

Taasisi ya afya ya Yohana Wavenza Mbozi imejidhatiti kutoa huduma za afya kwa kutoa elimu bora ya uuguzi, ugunduzi na mafunzo bora ya vitendo.

Lengo

Kutoa mafunzo bora kupitia wafanyakazi wenye uwezo na wenye kujituma wanaotumia mbinu zinazofaa katika mazingira mazuri.

Maadili

  • Ubora wa mafunzo na huduma za afya 
  • Ufanisi na utendaji wa shughuli
  • Mazingira ya kiutendaji
  • Huduma nzuri kwa wateja

Vivutio kutoka kwenye moja ya sherehe za kuhitimu

Utawala
MkuuMakamu Mkuu
Vitalis Rizick Magehema
Mediatrix Mwanjee


Mawasiliano

Taasisi ya afya ya Yohana Wavenza

S.L.P. 91
Mbozi-Songwe
Tanzania

Simu:     +255 764 486 922
Barua Pepe:  
yohanawavenzahealth@gmail.com


Kiswahili