Idara ya Uwakili

Neno Uwakili linatokana na neno la Kiebrania 'Ashurbeth' ambalo maana yake ni mtunzaji wa nyumba, mfano mzuri ni Yusufu katika nyumba ya Potifa (Mwanzo 39:1-9). Pia neno Wakili kwa Kiyunani ni Epitropos lenye maana ya 'Mwangalizi' au Aikonomia lenye maana ya Msimamizi wa Nyumba.

Kwa tafsiri hizi mbili neno Uwakili katika Kanisa maana yake ni uangalizi na usimamizi wa nyumba au usimamizi wa mali ya Kanisa. Sifa kuu ya Wakili ni kuwa mtunza siri za Mungu na mwaminifu (Warumi 12:3).

Katika Kanisa la Moravian Tanzania Jimbo la Kusini Magharibi, Katibu wa Idara ya Uwakili huteuliwa na Kamati tendaji miongoni mwa wachungaji.
WAJIBU WA WAKILI
1. Wakili ni msimamizi wa mali zote za jimbo.
2. Kutunza orodha ya mali ya Jimbo na kumbukumbu zote za mali.
3. Kukagua na kutembelea mali za Jimbo.
4. Kutoa mafundisho ya uwakili wa Kikristo kwa wakristo wote.
5. Kupokea na Kuchunguza taarifa ya maendeleo ya Idara kutoka viongozi wa Idara wa Wilaya.
6. Kupanga na Kuitisha warsha,Semina,kozi na mikutano mbalimbali.



Mch. Paul S. Mwambalaswa - Katibu wa Idara ya Uwakili KMT-JKM
Mawasiliano

Kanisa la Moravian Tanzania - Jimbo la Kusini Magharibi
Idara ya Uwakili 

S.L.P. 377
Mbeya
Tanzania

Barua Pepe: mwambalaswapaul@gmail.com
Simu:  +255 766505969 / +255 733587645
Kiswahili